Skip to main content

SALOME MAKAMBA AFUNGA MAONYESHO YA NISHATI EXPO 2026




Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini

Ayra Newstz, Dar

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam

Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. 

"Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba. 

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote.

Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanahama kutoka katika matumizi ya nishati zisizo safi na zisizo salama kwenda kwenye teknolojia bora za nishati safi ya kupikia.

Vilevile, Mha wa miradi Francis Manyama amemfafanulia  kuwa kupitia maonesho hayo, REA imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuonesha teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya kuni mbadala, majiko banifu, majiko ya umeme na teknolojia nyingine rafiki kwa mazingira.

Alieleza kuwa washiriki mbalimbali wakiwemo baba lishe, mama lishe, washiriki kutoka asasi za kirai, na mashirika ya binafisi, walimu na wadau wengine walitembelea banda la REA na kupata elimu pamoja na kujionea teknolojia hizo zinazochochea matumizi ya nishati safi nchini.

Aidha, Mha. Manyama alimueleza Mhe. Makamba kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi ya LPG ya kilo sita ipatayo 3,255 kwa kila Wilaya kwa lengo la kurahisisha upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Vilevile, alibainisha kuwa Wakala unatekeleza mradi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku, ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa ushirikiano na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na Jeshi la Magereza.

Katika hatua nyingine, alieleza kuwa REA kupitia TPDC imetekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia ya kupikia katika kaya zilizopo mikoa ya Lindi na Pwani, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi wa maeneo hayo. Pia alieleza kua Wakala kupitia STAMICO utawezesha usimikaji wa mashine ya kuzalisha mkaa mbadala katika mkoa wa Geita ili kurahisha upatikanaji endelevu wa nishati ya kupikia kwa wingi na wakati.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...