Skip to main content

MUHIMBILI, MEGA WE CARE YAWAFUATA WANANCHI HUDUMA ZA UCHUNGUZI, CHANJO YA HOMA YA INI BURE

 


Na Ayra Newstz 

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) imeanzisha kampeni maalumu ya siku mbili ya kutoa huduma za uchunguzi, chanjo na elimu kuhusu ugonjwa wa homa ya ini (Hepatitis), huku ikionya kuwa wagonjwa wengi hufika hospitalini baada ya ugonjwa kufikia hatua za hatari.

Kampeni hiyo, inayofanyika kwa ushirikiano na Mega We Care Tanzania Limited,ambapo imeanza Julai 28 na itahitimishwa Julai 29, 2026 katika IDC Clinic iliyopo karibu na Kituo cha Reli ya Kisasa (SGR) katikati ya Jiji la Dar es Salaam, huduma zote zinatolewa bila malipo kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Bingwa Mbobezi wa Magonjwa ya Ini wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Swaleh Kitabu Pazi, alisema hatua ya kupeleka huduma katikati ya jiji imelenga kuwafikia wananchi ambao mara nyingi hushindwa kufika hospitalini kutokana na majukumu yao ya kila siku.


Amesema kuwa, kliniki ya homa ya ini ya Muhimbili kwa sasa inawahudumia wagonjwa wapatao 5,000 waliosajiliwa, huku zaidi ya wagonjwa 100 wakifika kila siku kwa ajili ya matibabu na ufuatiliaji.

"Tunataka watu wajue hali zao mapema. Ugonjwa huu ukigundulika kwa wakati unaweza kudhibitiwa, lakini wengi wanafika hospitalini ukiwa tayari umeleta madhara makubwa," alisema Dkt. Pazi.

Alieleza kuwa homa ya ini aina ya B huambukizwa kupitia mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito au kujifungua, kujamiiana bila kinga, kuongezewa damu isiyo salama na matumizi ya vifaa vyenye ncha kali vinavyotumika na watu zaidi ya mmoja.


Aidha, aliwataka wananchi kuachana na imani potofu kuhusu ugonjwa huo, akifafanua kuwa hauambukizwi kwa kushikana mikono, kukumbatiana, mate, jasho wala kuishi nyumba moja na mgonjwa.

Kwa mujibu wa Dkt. Pazi, zaidi ya watu milioni 500 duniani wanaishi na maambukizi ya homa ya ini, huku takribani watu milioni 1.3 wakipoteza maisha kila mwaka kutokana na madhara ya virusi vya homa ya ini aina ya B na C.

Amefafanua kuwa, pamoja na ukubwa wa tatizo hilo, homa ya ini aina ya B inaweza kuzuilika kwa chanjo, wakati aina ya C inaweza kutibika endapo itagundulika mapema na mgonjwa kuanza matibabu kwa wakati.


Kwa upande wake, Afisa Habari wa Mega We Care Tanzania Limited, Mengi Ntasimba, amesema ushiriki wa kampuni hiyo katika kampeni hiyo ni sehemu ya mchango wake kwa jamii baada ya kuhudumu nchini kwa zaidi ya miongo miwili.

Ameongeza kuwa, kampuni imechangia vifaa vya uchunguzi, chanjo na dawa kwa watakaobainika kuwa na maambukizi, huku ikiendelea kushirikiana na taasisi za afya kuhamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara.

"Tunaamini kinga ndiyo msingi wa afya bora, kupitia kampeni hii tunataka wananchi wengi zaidi wapate fursa ya kujua afya zao na kupata huduma kwa wakati," alisema Ntasimba.


Naye, Mfanyabiashara wa Kariakoo, Joseph Daniel Chengula, mkazi wa Kimara Mwisho, alisema alipata taarifa za kampeni hiyo kupitia mitandao ya kijamii na kuamua kufika kupatiwa huduma.

Amesema kuwa, huduma zinatolewa kwa utaratibu mzuri na bila usumbufu, huku akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo kupima afya zao na kupata chanjo bila gharama.

Wataalamu wa afya wameendelea kusisitiza umuhimu wa uchunguzi wa mapema, chanjo na matibabu ya haraka, wakieleza kuwa hatua hizo ndizo njia bora ya kupunguza maambukizi na vifo vinavyotokana na ugonjwa wa homa ya ini nchini.


Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...