Skip to main content

WAZIRI MKUU MGENI RASMI UZINDUZI WA KITABU CHA “MAMA SAMIA DOCTRINE OF LAW”




Ayra newstz

Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania, TPBA, kimetangaza rasmi uzinduzi wa kitabu kipya cha “Falsafa ya Sheria ya Mama Samia” Mama Samia Doctrine of Law, sambamba na maandalizi ya Mkutano wake Mkuu wa Mwaka 2026.

Akizungumza na waandishi wa habari, Makamu wa Rais wa chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania TPBA, Debora Mcharo amesema kitabu hicho kinatoa mwangaza kuhusu mwelekeo na mafanikio ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Kitabu hiki ni muhimu sana kwa kila Mtanzania. Kinatueleza historia, falsafa na mafanikio ya nchi yetu chini ya uongozi wa Rais Samia. Tunawaomba wananchi wote wajitokeze kukisoma ili kuelewa vizuri mwelekeo wa nchi,”alisema Bi. Mcharo.

Bi. Mcharo amebainisha kuwa uzinduzi wa kitabu hicho unatarajiwa kufanyika tarehe 10 Julai 2026, saa 2:00 asubuhi,  katika Maktaba Mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (UDSM) na Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba.

Aidha, TPBA inatarajia kufanya Mkutano wake Mkuu wa Mwaka 2026 kuanzia tarehe 13 hadi 14 Julai 2026, katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC, Jijini Arusha,na katika Mkutano huo, Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Kwa mujibu wa Bi. Mcharo, mkutano huo utaiunganisha familia nzima ya Mawakili wa Serikali kutoka Tanzania nzima ili kutathmini utekelezaji wa majukumu kwa mwaka uliopita na kupanga mikakati thabiti kwa mwaka ujao.

“Mkutano huu ni jukwaa letu la kujipima, kubadilishana uzoefu na kuweka mipango itakayoiwezesha TPBA kuendelea kutoa huduma bora za kisheria kwa Serikali na wananchi,”alifafanua.

Kwa upande wake, Katibu wa chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) Rashid Mohamed Said, amesema uzinduzi wa kitabu hicho una umuhimu mkubwa kwa umma kwani unaeleza kwa kina falsafa ya utawala na sheria katika kipindi hiki.

“Nawaomba wananchi watenge muda na waje kusikiliza moja kwa moja yaliyomo katika kitabu hiki. Ni somo kubwa kwa taifa letu,” alisema Rashid.

Naye, Mweka Hazina wa TPBA,Andrew Kevela, amesema uzinduzi huo ni fursa ya kipekee kwa wananchi kukutana na viongozi mbalimbali wa Serikali. 

“Tunatarajia Mawaziri zaidi ya kumi kushiriki katika uzinduzi huu. Ni fursa kwa wananchi kuonana na viongozi wao na kupata uelewa mpana wa sera na sheria za nchi,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...