Skip to main content

ZAI FOUNDATION YATOA AJIRA KWA VIJANA WA KEKO, YAPANGA KUPANUA HUDUMA AFRIKA




 Na Mwandishi Wetu 

Wakati changamoto ya ukosefu wa ajira ikiendelea kuwaathiri vijana wengi nchini, Zain Foundation imeanza kuonekana kuwa chanzo cha matumaini kwa wakazi wa Kata ya Keko, wilayani Temeke, baada ya kuanza kutoa ajira na kuendesha programu za kuwawezesha vijana kujitegemea kiuchumi.

Akizungumza kuhusu shughuli za taasisi hiyo, Diwani wa Kata ya Keko na mmiliki wa kampuni ya Zain, Ismaili Said Amanzi, amesema tangu kuzinduliwa kwa Zain Foundation tayari vijana 10 wameajiriwa moja kwa moja, huku wengine wakinufaika kupitia programu mbalimbali za ukuzaji wa vipaji na ujasiriamali.

Amesema dhamira ya kuanzisha taasisi hiyo ni kuhakikisha vijana wanapata fursa za kujiajiri na kuendesha maisha yao bila kutegemea wengine.

"Lengo letu ni kuwainua vijana wa Keko na kuwafanya wajitegemee kiuchumi. Tunataka watoke kwenye utegemezi na waweze kujenga maisha yao kupitia kazi na vipaji walivyonavyo," amesema.

Kwa mujibu wa Amanzi, Zain Foundation ilianza Keko kwa makusudi ili wananchi wa eneo hilo wawe wa kwanza kunufaika na kampuni yao ya nyumbani kabla ya huduma hizo kusambazwa katika maeneo mengine.

Amesema kwa sasa Keko ina matawi matano ya Zeini Foundation, ambapo kila tawi lina vijana 10, hivyo jumla ya vijana 50 tayari wanashiriki katika programu mbalimbali zinazolenga kuwawezesha kiuchumi.

Mbali na kutoa ajira, amesema taasisi hiyo imeanza kuwasaidia vijana wanaotamani kuingia kwenye tasnia ya ubunifu kwa kuwapatia huduma za kurekodi maudhui bila malipo, huku ujenzi wa kituo cha mazoezi (gym) ukiendelea ili kukuza vipaji vya michezo na kuwahamasisha kushiriki shughuli halali za kujipatia kipato.

Amesema anaamini hatua hizo zitachangia kupunguza uhalifu miongoni mwa vijana na kuongeza ushiriki wao katika maendeleo ya Keko, Temeke na Taifa kwa ujumla.

Akizungumzia shughuli za kampuni yake, Amanzi amesema kampuni hiyo huzalisha zaidi ya bidhaa 150 za dawa za asili zinazolenga kusaidia watu wenye changamoto mbalimbali za kiafya.

Amesema bidhaa hizo hutengenezwa kwa kutumia malighafi za asili zinazopatikana Tanzania na kwamba kampuni inaendelea kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa kuzingatia taratibu zinazotakiwa.

Amesema kuwa, kuhusu mafanikio ya kampuni hiyo, Amanzi amesema bidhaa za kampuni hiyo, tayari zinasambazwa katika nchi mbalimbali za Afrika zikiwemo Angola, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Namibia.

Amesema kutokana na mchango wake katika sekta ya dawa za asili, ametunukiwa tuzo ya heshima nchini Angola, ambako pia amealikwa mwezi Oktoba kufanya mazungumzo ya kufungua kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za kampuni hiyo.

"Nimefarijika kuona bidhaa zinazozalishwa Tanzania zinapata heshima katika masoko ya kimataifa. Hii inaonyesha vijana wa Tanzania wana uwezo wa kushindana na kuleta heshima kwa nchi yetu," amesema.

Amanzi amesema uzoefu wake katika biashara za kimataifa unaonyesha kuwa mataifa mengi yanaendelea kutumia dawa za asili kwa kiwango kikubwa, jambo ambalo, kwa mtazamo wake, linapaswa kuwahamasisha Watanzania kuamini bidhaa zinazozalishwa nchini.

Akizungumzia kipindi cha mlipuko wa COVID-19, amesema Zain Company ilizalisha bidhaa za asili zilizotumiwa na baadhi ya wananchi katika kipindi hicho, huku akiishukuru Serikali ya wakati huo kwa kuhamasisha maendeleo ya tiba asili nchini.

Ametoa wito kwa Watanzania kuwa na uzalendo kwa kuunga mkono bidhaa zinazozalishwa nchini, akisema hatua hiyo itawasaidia wazalishaji wa ndani kupanua biashara zao na kufungua fursa zaidi za ajira kwa vijana.

"Tukiamini bidhaa zetu na kuwaunga mkono vijana wetu, watafika mbali, watafungua masoko mapya na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Tanzania. Tusikandamize juhudi za wazalishaji wa ndani, bali tushikamane kuwainua ili taifa letu linufaike," amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...