Skip to main content

KILA KILO INAYOPOTEA NI SHILINGI INAYOPOTEA - MENEJA FEDHA WA WMA ATOA SOMO NANE NANE


Na WMA - DODOMA.

Meneja wa Fedha wa Wakala wa Vipimo  (WMA), Bw. Ibrahim Mbinga, amesema usimamizi mbovu wa vipimo ndiyo adui mkubwa wa mfuko wa mfanyabiashara, mkulima na mnunuzi.

Akizungumza na wadau katika banda la WMA kwenye Maonesho ya 33 ya Nane Nane, Dodoma, Agosti 8, 2026 Meneja huyo amefafanua jinsi vipimo visivyo rasmi vinavyosababisha upotevu wa fedha usioonekana.

Mbinga ameeleza kuwa majukumu ya WMA yanalenga kuokoa wafanyabiashara, wakulima na walaji. “Watu wengi wanafikiri kupima kwa ndoo au visado ni rahisi. Lakini ukweli ni kwamba unajipiga risasi mguuni. Kila kilo, kila lita iliyopotea ni shilingi iliyotoka mfukoni mwako,” alisema.


Akidadavua kuhusu hesabu ya fedha kwenye vipimo, alisema vipimo ni sawa na mfuko wa fedha. “Gunia la mahindi kilo 100 ukiuza kwa ndoo 18 badala ya mizani, unapoteza kilo 10. Kama gunia ni shilingi 100,000, umepoteza shilingi 10,000. Ukiuza magunia 10 kwa wiki, umepoteza shilingi 100,000. Kwa mwezi ni milioni 1.2. Hiyo pesa ingekuwa wapi?” aliuliza.

Akieleza zaidi, alisema kuwa wafanyabiashara wengi hulalamika kupata hasara lakini akafafanua kuwa 'unaponunua mafuta lita 19 badala ya 20, au mpunga kilo 18 badala ya 20, unalipa pesa kamili na kupata bidhaa pungufu. Hiyo ni hasara ya moja kwa moja."


Akizungumzia mikopo kutoka Benki kwa wafanyabiashara wakulima alisema "Benki leo haziombi tu dhamana bali zinataka rekodi. Mkulima anayetumia mizani iliyohakikiwa na kuwa na risiti anaaminika zaidi. Vipimo sahihi vinakupa historia ya biashara yako ambayo benki inaitaka."

Aidha, Mbinga pia aliwaelimisha wafanyabiashara wakulima kuepuka gharama za faini ambazo husababisha hasara.

Akifafanua, alisema "kutumia vipimo visivyo rasmi ni kosa kisheria. Unapokamatwa unalipa faini na wakati mwingine bidhaa inaweza kuzuiliwa hivyo ni hasara mbili kwa wakati mmoja.

Badala yake, aliwashauri kuwekeza kiasi kidogo cha pesa kununua mizani iliyohakikiwa na WMA ili kujiepusha  na faini inayoweza kukuletea hasara.


Katika hatua nyingine, Mbinga aliwashauri wafanyabiashara wakulima 'kujenga jina' ili kupata faida stahiki. "Mteja anapojua kuwa kwako anapata haki yake, atarudi tena na tena na ataleta wengine. Hiyo inakupunguzia gharama ya kutafuta wateja. Uaminifu unalipa," alisisitiza.

Meneja huyo wa Fedha, alihitimisha kwa kusisitiza kaulimbiu ya WMA isemayo "Pima kwa Haki, Pata Faida Halali" akidadavua kuwa mfanyabiashara  akiwekeza kwenye mizani iliyohakikiwa leo, baada ya miezi miwili atashangaa tofauti yake kwenye akaunti yake ya fedha. 

Mbinga amewataka wadau pia kutumia risiti na vitabu vya mauzo vinavyotokana na vipimo sahihi ili kufuatilia kwa urahisi mapato na matumizi.


Kwa upande wao, Wadau wameipongeza WMA kwa kuleta wataalamu wa fani mbalimbali katika banda la maonesho ya Nane Nane na kusema elimu ya kifedha imewapa uelewa mpya.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...