Skip to main content

KIONGOZI MSTAAFU WA WMA ASEMA VIPIMO SAHIHI NDIYO MSINGI WA UCHUMI



Na WMA - DODOMA.

Kiongozi mstaafu wa Wakala wa Vipimo (WMA), aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Bw. Deogratius Aloyce Maneno amesema uwekezaji wa Serikali katika masuala ya vipimo ndiyo ufunguo wa kujenga uchumi imara na soko la haki.

Alisema hayo jana Agosti 8, 2026 alipotembelea banda la WMA kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima (Nane Nane), yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Dodoma.

Baada ya kupokelewa na wataalamu wa WMA na kupewa maelezo ya maboresho mapya ya vifaa na elimu ya vipimo, Mkurugenzi Mstaafu alisema anajivunia kuona kazi aliyoshiriki kuianzisha ikiendelea na kukua.

“Nimefurahishwa sana kuona WMA imepiga hatua kubwa. Tulipoanza tulikuwa na changamoto za vifaa na uelewa, lakini leo naona vijana wanasimama wenyewe kutoa elimu. Hii ndiyo tija ya uwekezaji,” alisema.

Kutokana na uzoefu wake wa miaka mingi WMA, kiongozi huyo alitoa ushauri katika maeneo kadhaa ili kuboresha zaidi huduma za uhakiki wa vipimo.

 Kwanza, alisema kuwa ni jambo jema kutoa elimu kwa wafanyabiashara wakubwa. Hata hivyo alisisitiza kuwa "huu ni wakati wa kushuka ngazi hadi kwa mama lishe na wauuzaji wa sokoni maana ndio wanaoumia zaidi na vipimo visivyo rasmi,” alisema.

Pia, 'Bosi Deo' kama wengi wanavyomwita alitoa ushauri kwa wafanyabiashara kukumbatia teknolojia akisema kuwa “Dunia imebadilika. Tumieni mizani ya kidijitali zaidi na mifumo ya kutoa risiti. Hii itasaidia kuwa na rekodi na kupunguza ubadhilifu katika biashara.”

Aidha, alitoa ushauri kwa watendaji wa WMA kutokuogopa kutumia sheria inayoingoza Wakala kuwabana wale wanaokiuka maelekezo na taratibu halali za kivipimo. 

“WMA ina mamlaka. Itumieni. Mkikamata na kutoa faini kwa wale wanaokiuka, wengine watafuata sheria. Soko la haki linahitaji nidhamu.”

Kwa upande wake, Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa WMA, Bi. Veronica Simba, alimshukuru kiongozi huyo mstaafu kwa kuwa sehemu ya walioweka misingi imara ya utendaji kazi WMA.

“Tunajivunia alama ambayo wewe pamoja na wastaafu wengine mliiweka. Leo tunaendeleza dira yenu ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata kipimo sahihi. Milango yetu iko wazi kwa ushauri wako wakati wote,” alisema.

Wananchi waliokuwepo bandani walifurahishwa na uwepo wa kiongozi huyo mstaafu na kusema ni mfano mzuri wa watu kurejea kutoa uzoefu kwa vizazi vipya.

Wastaafu wengine waliotembelea banda la WMA kwenye Maonesho ya NaneNane ni pamoja na Bw. Evarist Masengo aliyekuwa Meneja wa WMA ngazi ya Mkoa na Bw. Joseph Maliti aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi. Wote walikiri kufurahishwa na maendeleo ya Wakala na waliupongeza Uongozi uliopo pamoja na wafanyakazi wote kwa ujumla.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...