Skip to main content

TIRDO YALEA UBUNIFU WA VIWANDA, YASUKUMA TEKNOLOJIA ZA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO

 


Na Ayra News 

Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limesema linaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kuongeza thamani ya mazao ya kilimo, hatua inayolenga kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvunwa na kuongeza kipato kwa wakulima na wajasiriamali.

Akizungumza katika Maonyesho ya Nanenane 2026,Mtaalam na Mtafiti wa Teknolojia za Nishati, Mhandisi Augustino Masse kutoka TIRDO alisema shirika hilo linaimarisha mnyororo wa thamani wa mazao kupitia utafiti, ubunifu na teknolojia zinazosaidia mazao kudumu kwa muda mrefu bila kupoteza ubora wake.

Alisema kuwa, tafiti zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 40 ya mazao yanayoharibika kwa haraka, yakiwemo nyanya, matunda na mboga za majani, hupotea kutokana na ukosefu wa teknolojia sahihi za uhifadhi na usindikaji.

Kutokana na hali hiyo, TIRDO imeendelea kuhamasisha matumizi ya makaushio yanayotumia nishati ya jua, teknolojia inayowezesha mazao kukauka kwa viwango vinavyokubalika huku yakihifadhi ubora, virutubisho na kuongeza muda wa kuhifadhi.


Mhandisi Masse alisema kila zao lina mahitaji yake ya kitaalamu katika mchakato wa ukaushaji, hivyo TIRDO imebuni makaushio yanayozingatia kiwango cha joto na muda unaohitajika kwa kila zao ili kuhakikisha ubora wa bidhaa unaendelea kubaki.

Mbali na teknolojia za ukaushaji, alisema shirika hilo linaendelea kuhimiza matumizi ya nishati mbadala kwa kuhamasisha mabaki ya mazao ya kilimo kutumika kuzalisha nishati, hatua inayosaidia kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa pamoja na kuhifadhi mazingira.

Alibainisha kuwa TIRDO tayari imewezesha ujenzi wa makaushio zaidi ya saba katika maeneo mbalimbali nchini, huku mradi mwingine ukiendelea kutekelezwa Mbagala jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa Mhandisi Masse, jukumu la TIRDO si kutengeneza bidhaa kwa ajili ya kuziuza sokoni, bali ni kulea na kuendeleza wabunifu na wajasiriamali kwa kuwapatia ushauri wa kitaalamu, teknolojia na mbinu za uzalishaji ili bidhaa zao zikidhi viwango vya ubora kabla ya kuwasilishwa kwa mamlaka za udhibiti na uthibitishaji kama Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Aliongeza kuwa kupitia huduma za incubation, TIRDO imeendelea kuwajengea uwezo wabunifu wengi wa Kitanzania kubadilisha mawazo yao kuwa bidhaa zenye thamani ya kibiashara, hatua inayochochea ukuaji wa viwanda na kuongeza mchango wa sekta ya kilimo katika uchumi wa taifa.

Aidha, aliwataka wakulima, wajasiriamali na wananchi wanaotembelea Maonyesho ya Nanenane 2026 kutembelea banda la TIRDO ili kujifunza teknolojia mbalimbali zinazotolewa na shirika hilo, zikiwemo za kuongeza thamani ya mazao, matumizi ya nishati mbadala na fursa za kulea bunifu zinazoweza kugeuka kuwa biashara zenye tija.


Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...